Jumapili, 23 Aprili 2017

JUMATAU YA PASAKA 2017

IBAADA YA JUMATATU YA PASAKA TAREHE 17.04.2017
MHUBIRI: MCHUNGAJI MARY MNEO
MAANDIKO: WAEBRANIA 2:3
UJUMBE: KUJALI.
Tutapataje kupona tusipojali wokovu mkuu namna hii? Yesu aliicha  enzi yake na kuja dunia kwa ajili ya ukombozi wa mwanadamu yaani mimi na wewe. Si hivyo tu pia alikubali kuchukuwa mateso yetu. Yeye wala hakustahili kupata mateso yale aliyoyapata msalabani. Ni upendo wake kwa ajili yetu. Wakati mwingine hatujali huu wokovu ambao hupatikana mara moja tu. Tunaweza kufanya tunayoyataka kwa kutojali wokovu ambao Yesu alijitoa hata kuutoa uhai wake pale msalabani. Alisema Baba imekwisha pale kalivari. Unapotafakari upendo wa Yesu kwa ajili yetu hasa tunaposikia ujumbe huu wa tutapataje kupona tusipojali wokovu mkuu namna hii? Tuijali kazi kubwa ambayo Yesu aliifanya pale msalabani ili tupate kuwa haki ya Mungu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni