Jumapili, 21 Mei 2017

SAA YA TAABU YAKO INAPITA

SAA YA TAABU YAKO INAPITA
2WAFALME 4: 1 -7 
Tarehe 21.05.2017

Saa ya taabu inapofika huumiza, huteta majuto, huteta maswali mengi, huleta manung`uniko, huwa na uchungu, hukosesha amani moyoni, huondoa furaha nakadhalika. Kwa upande wa mtu wa Mungu saa ya taabu inapofika huweza kumwondoa katika uwepo wa Mungu.

Mwanamke mmoja miongoni mwa wake za wana wa manabii alimlilia Elisha kwa habari za watoto wake wawili  kutaka kuchukuliwa ili wawe watumwa. Huyu mama alifiwa na mmewe na hakuwa na mali nyingi za kukidhi haja maisha yake ya kila siku. Yumkini alikuwa na madeni mengi hata yakampelekea kushindwa kulipa. Hakika ilikuwa saa ya taabu yake. Lakini Mtumishi wa Mungu Elisha alipofika nyumbani kule mama, mama yule akamwambia habari za watoto wake kutaka kuchukuliwa kuwa watumwa. Elisha akamwambia wataka nikufanyie nini? Niambie una kitu gani nyumbani? Mama yule akajibu akasema mimi ni mjakazi wakosina kitu nyumbani ila chupa ya mafuta. Ndipo Elisha akamwambia akisema nenda ukatake vyombo huko nje kwa majirani zako wote vyombo vitupu wala usitake vichache. Kisha uingie ndani ukajifungie mlango wewe na wanao ukavimiminie mafuta vyombo vile vyote. Mama yule akafanya hivyo ndipo vyombo vyote vikajaa mafuta. Biblia inatuambia vyombo vilipokuwa vimejaa Mtumishi Elisha akamwambia mama niletee tena chombo. Mama akajibu akisema hakuna tena chombo. Hivyo mama yule saa ya taabu yake ikawa mwisho kwani mafuta yale aliyauza na kulipa manedi ili watoto wake waliende utumwani

Ndugu saa ya taabu yako inapita tu. Kwa nini kufadhaika, kuhangaika na hata kuvunjika moyo kwa taabu yako unayoipita. Kumbuka saa ya taabu inapita tu. Yesu yupo alipigwa msalabani kwa ajili ya taabu yako. Usimwache Yesu kwa taabu yayo unayoipitia. Ayubu hakumwach aMungu kwa taabu yake aliyoipata. Mweleze Yesu taabu yako naye atakutokea. SAA YA TAABU INAPITA USIOOGOPE.

Mhubiri
Mchungaji. Mary Mneo

KUNA NGUVU KATIKA NENO LA MUNGU

UJUMBE: KUNA NGUVU KATIKA NENO LA MUNGU
LUKA 5: 4 -11
Tarehe 14.05.2017

Luka aliandika habari zake baada ya kufanya utafiti wa jambo analotaka kuliandikia kama taaluma yake ya utabibu ambapo inamtaka kufanya uchunguzi kwanza kabla ya kutoa tiba kwa mgonjwa.  Luka aliandika habari za Yesu na Simoni Petro kuhusu kushusha nyavu hadi kilindini ili wakavue samaki. Maandiko yanatuambia kuwa wakati Yesu anakutana na akina Simoni Petro muda wa kuvua samaki ulikuwa umepita na walikwisha kuosha nyavu zao ili warudi nyumbani kwani kwa kazi ya usiku ule haikuwa na mafanikio kwa kuwa hawakupata samaki. Ndipo Yesu akawaambia shusheni nyavu zenu mpaka kilindini mkavue samaki. Simoni Petro akajibu Bwana tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha tusipate kitu lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu. Basi wakaenda mpaka kilindini wakashusha nyavu zao mara nyavu zao zikaanza kuzama kwa wingi wa samaki wakaamua kuwaita washirika wenzao ili wasaidiane kuchukua samaki. Wakapata samaki wengi sana.

Hebu tuone nguvu ya kuliamini Neno la Mungu
Simoni Petro aliposema kwa Neno lako nitazishusha nyavu kwani alitambua kuwa kazi yao ya usiku kucha haikuwa na mafanikio na wao mahitaji yao yalikuwa ni kupata kitoeo na matumizi mengi kwa familia. Walichoka sana kwa kazi hiyo ya usiku kucha lakini wakaamua kulitii Neno la Mungu na kulitendea kazi kwa kushusha nyavu kama Bwana alivyosema. Je mimi na wewe leo tunaweza kufanya hivyo. Mbona ujumbe unapokuja kwako unaona si wako ila wa mtu mwingine? Hatupokei kutoka kwa Bwana kwa kutoliamini Neno la Mungu.

Ipo nguvu katika kuliamini Neno la Mungu. Neno la Mungu huleta matokeo chanya katika maisha ya mwamini ukiliamini sawa sawa na Neno lake.


Mhubiri
Mchungaji Kiongozi: P. Mneo

KILELE CHA JUMA LA CMF: CHANGAMKA USIOOPE

Ujumbe: Changamka usiogope
Marko 6: 45 - 51

Yesu aliwalazimisha wanafunzi wake wapande mashuani na kuanza safari ya kuvuka ng`mbo hata Bethsaida. Yesu akabaki na makutano kwa kitambo kidogo. Wanafunzi wakaanza safari yako kwenda Bethsaida. Na kulipokuwa jioni mashua ilikuwa katikati ya bahari na Yesu yu pekee yake katika nchi kavu akawaona wanafunzi wake wakitaabika kwa kuvuta makasia kwa maana upepo ulikuwa wa mbisho hata ilipopata zamu ya saa nne ya usiku Yesu akawendea akitembea juu ya bahari. Wanafunzi walipomwona walidhani ni kivuli wakapiga yowe kwa kuwa wote walimwona wakafadhaika. Mara akasema nao akawaambia " Changamkeni ni mimi hapa msioogope". Akapanda chomboni upepo ukakoma.

Mpendwa hata kama unapita katika magumu ya namna gani usioogope Yesu yupo kwa ajili yako anakuona ukitaabika hivyo mwamini yeye naye atakutokea katika majaribu yako CHANGAMKA USIOGOPE

Mhubiri
Ndg Donalth Kweka
Mwenyekiti CMF

YESU NDIYE SULUHISHO LAKO

UJumbe: YESU NDIYE SULUHISHO LAKO
Maandiko: Luka 5:12 - 14
Tarehe 30.04.2017

Ukoma katika jamii ya Israel ilikuwa ni tatizo kubwa mno. Mtu mwenye ukoma ililazimika kutengwa  kama tunavyosoma maandiko Mambo ya Walawi 13 - 14.

Hata sasa dunia huwatenga watu wenye ukoma. Ukoma hushambulia mwili na hata mfumo wa fahamu. Kwa zama za Agano la Kale mtu mwenye ukoma alitengwa kwa muda fulani mpaka atakapotasika na baada ya kutakaswa atoe sadaka maalumu. Kuhani alihusika kumkagua mtu mwenye ukoma kama ametakasika au la. Mtu mwenye ukoma akichangamana na watu wasio na ukoma sheria iliwaruhusu kumwua mtu huyo kwa mawe. 

Siku moja mwenye ukoma alisikia habari za Yesu na akazimia moyoni mwake kwenda kwake ili aponywe na ukoma. Ugonjwa huo ulimtesa kwa siku nyingi akaanguka kifudifudi mbele za Yesu akisema " Bwana ukitaka waweza kunitakasa". Ndipo Yesu akaunyoosha mkono wake akisema nataka takasika. Mara mtu mwenye ukoma wake ukamwondokea. 

Imani ya mtu mwenye ukoma ilimfanya atakasike na akawa huru kuchangamana na watu wengine

Mtu wa Mungu ukoma ni dhambi ambayo hutufanya tufarakane na Mungu. Ni kitu gani kwako ambacho ni ukoma kinakufanya usipokee muujiza wako? Nenda mbele za Bwana umweleze mambo yako na akurehemu ndipo upokee haja ya moyto wako kama vile mtu yule aliyekuwa na ukoma alipomwendea Yesu na kuanguka kifudifudi.


Mhubiri
Mchungaji Jonas Charles Shebila
T.A.G Michungwani Muheza