Marko 6: 45 - 51
Yesu aliwalazimisha wanafunzi wake wapande mashuani na kuanza safari ya kuvuka ng`mbo hata Bethsaida. Yesu akabaki na makutano kwa kitambo kidogo. Wanafunzi wakaanza safari yako kwenda Bethsaida. Na kulipokuwa jioni mashua ilikuwa katikati ya bahari na Yesu yu pekee yake katika nchi kavu akawaona wanafunzi wake wakitaabika kwa kuvuta makasia kwa maana upepo ulikuwa wa mbisho hata ilipopata zamu ya saa nne ya usiku Yesu akawendea akitembea juu ya bahari. Wanafunzi walipomwona walidhani ni kivuli wakapiga yowe kwa kuwa wote walimwona wakafadhaika. Mara akasema nao akawaambia " Changamkeni ni mimi hapa msioogope". Akapanda chomboni upepo ukakoma.
Mpendwa hata kama unapita katika magumu ya namna gani usioogope Yesu yupo kwa ajili yako anakuona ukitaabika hivyo mwamini yeye naye atakutokea katika majaribu yako CHANGAMKA USIOGOPE
Mhubiri
Ndg Donalth Kweka
Mwenyekiti CMF
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni