Jumapili, 26 Machi 2017

IBAADA YA MEZA YA BWANA

IBAADA YA MEZA YA BWANA TAREHE 26.03.217
Ibaada hii imefanywa na Mchungaji Kiongozi P. Mneo

Maandiko 1Kor 11: 24 - 32

Matukio katika picha.


Mchungaji Kiongozi akitoa ujumbe wa Meza ya Bwana
Mchungaji Mary Mneo akiombea mkate


Mzee wa kanisa ndg Frida Kweka akiombea divai

Viongozi wakiwa tayari kuhudumu meza ya Bwana





JE UMEIMIMINA ROHO YAKO KWA NANI?

IBAADA YA TAREHE 26.3.217
MHUBIRI: Ndg VERONICA MALUWA
UJUMBE: Je umeimimina roho yako kwa nani?
Maandiko: 1Samwel 1: 9 - 20





1Samwel 1:15 ( ......... mimi sikunywa divai wala kileo ila nimeimimina roho yangu mbele za Bwana).

Utangulizi: 
Kumimina roho kwa Bwana ni ile hali ya kupeleka au kueleza haja ya moyo kwa Mungu kwa unyenyekevu mkuu. 

Palikuwa na mtu mmoja mcha Mungu aliyeitwa Elkana. Naye Elkana alikuwa na wake wawili mmoja aliitwa Hana na wa pili aliitwa Penina. Penina alikuwa na watoto lakini Hana hakuwa na mtoto kwa wakati ule kwa Mungu alimfunga tumbo lake kwa muda. Moyo wa Hana ulikuwa na huzuni kwa kukosa mtoto ndipo akaamua moyoni mwake kuimimimna roho yake kwa Bwana. Mungu akasikia haja ya moyo wake hatimaye akapata mtoto wa kiume akamwita jina Samwel.

Ujumbe 
Katika maisha yetu ya kila siku yapo mahitaji mbalimbali na mengine ni magumu kwetu lakini ukiimimina roho yako kwa Bwana naye atafanya kwa ajili yako. Yeye ni mwaminifu ukitembelea pamoja naye kama Hana alivyofanya.

Faida ya kuimimina roho yako kwa Bwana
  1. Bwana atakulinda (Mdo 16: 25) 
  2. Bwana atakuinua  (Mwanzo 41: 45)
  3. Kwake yeye ni kimbilio na nguvu (Zab 46:1)
Hitimisho
Inawezekana mpendwa hupokei haja ya moyo wako kwa kuwa hujaimimina roho yako kwa Bwana. Mimina haja ya moyo wako kwa Bwana naye atakutokea. Kwa Mungu wetu hakuna jambo asiloliweza tazama mfano wa Shadrack, Meshack na Abedinego katika tanuri la moto Mungu alichowafanyia. Tusikate tamaa wala kumtenda Mungu dhambi. 

IBAADA YA KUWAWEKA WAKFU WATOTO

IBAADA YA KUWAWEKA WAKFU WATOTO TAREHE 26.03.2017


Matukio katika picha. Tazama picha hapa chini









Jumapili, 19 Machi 2017

NANYI MWANINENA KUWA MIMI NI NANI?

IBADA YA TAREHE 19.03.2017
MHUBIRI: NDG DICKSON A. MFIKWA
UJUMBE: Nanyi mwaninena kuwa mimi ni nani?

Maandiko: Math 16: 13 - 16













Utangulizi
Kitabu cha kwanza kabisa katika Agano Jipya ni kitabu cha Injili ya Mathayo. Kitabu hiki kinasadikiwa kiliandikwa na Mathayo Mwenyewe kwenye mwaka 65 - 70 BK. Lengo la kuandikwa  kwa kitabu hiki ilikuwa kuthibitisha kuwa Yesu Kristo ni Masihi wao wa kweli.

Somo lenyewe.
Maana ya Masihi au Masiya:
   Mtu anayeaminiwa na wakristo kuwa ni Mwana wa Mungu aliyezaliwa kuwaokoa watu dhidi ya dhambi, Mkombozi, Yesu Kristo (kwa mujibu wa kamusi ya Kiswahili sanifu).

Siku moja Yesu akaamua kuwauliza wanafunzi wake kuhusu maisha yake akitaka kufahamu hasa watu wanamnenaje kuhusu yeye mwenyewe. Kwa maana nyingine aliamua kufanya tathmini ya maisha yake. Kupitia maisha au huduma ya Yesu Kristo aliyokuwa akifanya watu walimnena kuwa yeye huhenda ni Yohana Mbatizaji, Elia, Yeremia au miongoni mwa Manabii. Hivyo ndivyo wanafunzi walivyojibu swali ambalo Yesu Kristo alilouliza. Yesu hakuishia hapo akawauliza tena wanafunzi nanyi mwaninena kama mimi ni nani? Ndipo Petro akajibu kuwa wewe ni Mwana wa Mungu aliye hai.

Zipo sababu zizowafanya watu wengine waseme kuwa Yesu Kristo ni Yohana Mbatizaji, Elia, Yeremia au ni miongoni mwa Manabii. Kati ya sababu hizo ni nguvu alizokuwa nazo Yesu Kristo katika huduma yake kama vile vipofu waliona, viwete walitembea, wenye ukoma walitakasika, wafu walifufuka, wenye mapepo walitolewa, wagonjwa walipata nguvu nakadhalika.

Maisha mkristo wa leo
Nasi katika maisha tunayoyaishi hatuna budi kujifanyia tathmini kama Bwana wetu Yesu Kristo alipoamua kujitathmini juu ya maisha yake kwa watu waliokuwa wakimzunguka pamoja na wanafunzi wake. Leo maisha yetu yamezuia nguvu za Mungu kutendeka ndani ya kanisa kwa sababu ya ushuhuda wa maisha yetu kwa watu waliopo ndani na nje ya kanisa. Inatupasa kufanya tathmini ya maisha yetu ili tuweze kubalika na kumlingana Bwana wetu Yesu Kristo. Tuone ni wapi tunakosea na kutubu kama Isaya alivyofanya (Isaya 6:5). Matendo, Maneno na mawazo yawe safi mbele za Mungu.

Madhara ya kutenda dhambi

  1. Utasababisha hata asiye na hatia kuangamia kwa ajili yako. (Yoshua 7: 1, 5, 20, 24)
  2. Nguvu za Mungu hazitendi kazi ndani yetu

Hitimisho. 
Mpendwa tukitaka nguvu za Mungu zitende kazi ndani yetu na watu wengine waokolewe hatuna budi kuacha kutenda dhambi na kuishi maisha yenye ushuhuda mzuri mbele za Mungu.




Jumapili, 12 Machi 2017

MUNGU HUSIMAMA NA MWENYE HAKI

IBADA YA TAREHE 12.03.2017

MHUBIRI: MCHUNGAJI MARY MNEO
UJUMBE: Mungu husimama na mwenye haki


Mchungaji Mary Mneo akihubiri
Mambo tunayojifunza katika Mwan 6: 1 - 13 ni kama ifuatavyo:-

  1. Mtazamo wa wana wa Mungu haukuwa kama Mungu alivyokusudia.
  2. Mungu anaweka hisia zake wazi juu ya kutoshindana na mwanadamu
  3. Mungu anayaona mawazo ya mwanadamu kuwa ni mabaya siku zote.
  4. Nuhu anapata neema machoni pa Mungu.
Kilichomfanya Nuhu kupata neema machoni pa Mungu katika dunia iliyojaa dhuluma ni kutembea pamoja na Mungu.

Hitimisho: Hata sasa mtu wa Mungu fanya maamuzi ya kutembea pamoja na Mungu. Haijalishi tupo kwenye dunia ya namna gani bado tunaweza kupata neema machoni pa Mungu kama ilivyokuwa kwa Nuhu.


IBADA YA KUWAWEKA WATOTO WAKFU KWA MUNGU

Mchungaji na wazazi wenye watoto wa kuwekwa wakfu kwa Mungu


Mchungaji akipoke mtoto kutoka kwa mzazi

Mchungaji Kiongozi akiombea mtoto



 Hizi ni baadhi ya picha katika matukio ya ibada ya kuwaweka watoto wkfu kwa Mungu.

Jumapili, 5 Machi 2017

KILELE CHA JUMA LA WWK 2017


Tarehe 5.3.2017
KILELE CHA JUMA LA WWK
MHUBIRI: M/KITI NDG FRIDA KWEKA

Mwenyekiti WWK akitoa ujumbe


 UJUMBE: JE WATAKA KUPONA?
Ebr 2:3, Yoh 5:24, Fil 3:7 - 8 na Yuda 1:3

Ili tuweze kupona hatuna budi kufanya yafuatayo


      1. Kufanya mambo ya Mungu kwanza halafu yetu baadaye.
      2. Kuvaa silaha za Mungu. (Efe 6: 10 - 18).
      3. Kujitambua











MATUKIO KATIKA PICHA

Viongozi wa WWK wakiwa mbele ya Madhabahu

WWK wakiimba wimbo wao

Hawa ni WWK wakiongoza Ibada ya sifa na kuabudu


Mchungaji na Mama Mchungaji

Familia ya Mchungaji


Mchungaji na mama Mchungaji wakipokea zawadi kutoka kwa Mwenyekiti wa WWK